1992

Mwaka wa Kusajiliwa Rasmi

200+

Misikiti na Mazawiya

400+

Vyuo vya Qur'ani

26

Mikoa ya Tanzania

JZQT

Kumjua Mola wetu na kupata radhi zake kupitia malezi ya Twariqa.

Karibu

JZQT ni Nini?

Jumuiya Zawiyatul Qadiriya Tanzania (JZQT) ni Jumuiya ya Kidini iliyosajiliwa nchini Tanzania, inayofuata Twariqatul Qadiriya. Tangu tulipoanzishwa, tumejikita katika kuhifadhi na kueneza mafundisho ya Kiislamu kama yalivyopokelewa kupitia Qur'ani na Sunna, tukisimamia Misikiti, Mazawiya na Vyuo vya kufundishia Qur'ani na malezi ya Ki-Twariqa katika mikoa mbalimbali ya Tanzania Bara, Unguja na Pemba.

Kupitia tovuti hii unaweza:

Kujiunga kuwa Mwanachama

Kufuatilia Habari na Matukio

Kusoma Vitabu na Kusikiliza Darsa

Kuchangia Miradi ya Jumuiya

Soma Zaidi Kuhusu Sisi Jisajili
Safari Yetu

Historia ya JZQT

Kuanzia jitihada za mwanzo hadi Jumuiya inayotambulika nchini kote.

1980

Jitihada za mwanzo za kuianzisha Jumuiya zaanza.

1988

Usajili wa awali Arusha kwa jina "Masjid Zawiya El-Qadiriya".

1990

Usajili rasmi na Wizara ya Mambo ya Ndani (S.O.7168).

1991

Mkutano Mkuu Arusha wabadilisha jina kuwa JZQT.

1992

Usajili wa mwisho wakamilika na Jumuiya yatambulika rasmi.

Blog na Habari

Taarifa Mpya

Rais wa Zanzibar Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi Akutana na Uongozi wa JZQT Ikulu Zanzibar
Habari
Rais wa Zanzibar Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi Akutana na Uongozi wa JZQT Ikulu Zanzibar

04 Aug 2026

Rais wa Zanzibar Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi amekutana Ikulu Zanzibar na ujumbe wa viongozi wa JZQT ukiongozwa na Mlezi wao mpya, Sheikh Ali Juma Mpwani, wakiambatana na Kadhi Mkuu wa Zanzibar.

Soma Zaidi
Kumtambulisha Mlezi Mpya wa JZQT: Sheikh Ali Juma Mpwani Alqadiriy
Habari
Kumtambulisha Mlezi Mpya wa JZQT: Sheikh Ali Juma Mpwani Alqadiriy

19 Jul 2026

JZQT inafuraha kumtambulisha rasmi Sheikh Ali Juma Mpwani Alqadiriy kama Mlezi mpya wa Jumuiya.

Soma Zaidi
Taarifa ya Msiba: Kuondokewa na Mlezi Sheikh Sayyid Othman bin Abdulqadir Albarawiy Alqadiriy
Habari
Taarifa ya Msiba: Kuondokewa na Mlezi Sheikh Sayyid Othman bin Abdulqadir Albarawiy Alqadiriy

19 Jun 2026

Inna lillahi wa inna ilayhi raji'un. JZQT inatangaza kuondokewa na Sheikh Mlezi wetu mpendwa, Marehemu Sheikh Sayyid Othman bin Abdulqadir Albarawiy Alqadiriy.

Soma Zaidi
Fahamu Zaidi

Maneno Muhimu ya Ki-Twariqa

Bofya kila kichwa hapa chini kusoma maelezo zaidi.

Dini ya Kiislamu imegawanyika sehemu kuu mbili: Sharia (Fiqhi) — elimu ya Ibada za kimwili kama Swala, Zaka, Funga na Hija; na Twariqa (Tasawwuf) — elimu ya Ibada za Kiroho. Mafundisho haya mawili yanakamilishana: Sharia bila Twariqa hukosa ukamilifu wa Kiroho, kwani Ibada za kiwiliwili peke yake haziitoshelezi nafsi bila kuisafisha Moyo.

Kwa maana ya Kidini, Twariqa ni mwenendo wa Ibada ulio bora, mwepesi na wa haraka zaidi wa kumfikia Mwenyezi Mungu (S.W). Kazi yake ni kushughulikia Ibada za Kiroho - kumfundisha Muislamu kumpenda sana Mwenyezi Mungu na Bwana Mtume Muhammad (S.A.W), kumuondoshea tabia mbaya kama kiburi, hasadi, ghadhabu na chuki, na kumjengea moyo safi wenye unyenyekevu, subira na mapenzi kwa Muumba na viumbe wenzake.

Ijaza ni njia rasmi ya kuipata Twariqa — aina ya ahadi (Mubayaa) anayoichukua Muridi mbele ya Sheikh wake ya kufungamana na Ibada ya Mwenyezi Mungu (S.W). Asili yake inatokana na tukio la Sayyidina Ali bin Abi Twalib (K.W) alipomuomba Bwana Mtume Muhammad (S.A.W) njia iliyo fupi, bora na nyepesi zaidi ya kumfikia Mwenyezi Mungu; akapewa jibu "Laa ilaha illa Llahu" kwa uongozi wa Sayyidina Jibril (A.S). Tangu wakati huo, Ijaza imekuwa ikitolewa mkono kwa mkono kutoka kizazi kimoja hadi kingine, hadi leo. Kwa maelezo zaidi kuhusu hali yako ya Ijaza, angalia sehemu ya Wasifu baada ya kujisajili.

Zawiya ni mahala maalum kwa ajili ya malezi ya Kidini, hasa kwa kumtaja na kumkumbuka Mwenyezi Mungu (Dhikr). Zawiya la kwanza katika historia ya Uislamu ni Pango la Hira (Makka), alipokuwa akidhikiri sana Bwana Mtume Muhammad (S.A.W) kabla ya kupewa Utume. Leo, neno Zawiya linatumika kuelezea mahali ambapo Muridi (wafuasi wa Twariqa) hukusanyika kwa ajili ya mafunzo na malezi ya Kidini.
Michango

Changia Jumuiya

Ujenzi wa Msikiti Mpya - Kinondoni

Tunachangisha fedha kwa ajili ya ujenzi wa msikiti mpya utakaohudumia jamii ya Kinondoni. Kila mchango wako una thamani...

TZS 18,501,000 kati ya TZS 50,000,000

Changia Sasa
Msaada wa Elimu kwa Watoto Yatima

Mchango huu utasaidia ada na vifaa vya shule kwa watoto yatima wanaotambuliwa na Jumuiya.

TZS 6,200,000 kati ya TZS 15,000,000

Changia Sasa
Mali za Jumuiya

Misikiti na Mali Zetu

Msikiti Mkuu wa Kinondoni
Msikiti Mkuu wa Kinondoni

Masjid

Angalia Zaidi
Zawiya Kuu ya JZQT
Zawiya Kuu ya JZQT

Masjid

Angalia Zaidi
Kiwanja cha Ilala
Kiwanja cha Ilala

Land

Angalia Zaidi