RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi akikabidhiwa picha maalum ikimuonesha Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Alhajj Ali Hassan Mwinyi alipofika hospitali kumuangalia Hayati Sheikh Muhammad Nassor Abdallah alipokua amelezwa Hospitali akipata matibabu, baada ya kumalizika kwa Ibada ya Sala ya Ijumaa na Kisomo cha Dua cha kumuombea Rais Mstaafu wa Tanzania Hayati Alhajj Ali Hassan Mwinyi, iliyofanyika katika Masikiti Ngamia Welezo Wilaya ya Magharibi
Soma ZaidiRAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi akisalimiana na kuagana na Mlezi wa Jumuiya ya Zawiyatul Qadiriya Tanzania Sheikh.Said Othman, baada ya kumalizika kwa Ibada ya Sala ya Ijumaa na Kisomo cha Dua ya kumuombea Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Awamu ya Pili Hayati Alhajj Ali Hassan Mwinyi, iliyofanyika katika Msikiti Ngamia Welezo Wilaya ya Magharibi
Soma ZaidiTunamshukuru Mwenyezi Mungu (S.W) kwa kutupa uzima na afya
pamoja na kutujaalia uwezo wa kupata Jumuiya yetu hii, JUMUIYA ZAWIYATUL QADIRIYA TANZANIA.
Ili kudumisha umoja wetu KI-DINI katika misingi imara zaidi, tumeamua kuunda Jumuiya ya kutuwezesha
kuendeleza umoja wetu kihalali kwa faida zetu, vizazi vyetu vya sasa na vya baadaye na Waislamu wote.
Katika zama hizi tulizonazo, hali halisi ya Waislamu katika elimu ya Dini, Imani, ucha Mungu, na uongozi wa Dini ni duni sana.
Kwa hiyo, sisi wafuasi wa Twariqa ya Qadiriya hapa Tanzania tumeamua kujitambulisha rasmi kwa Serikali zetu na kwa Waislamu
wenzetu kote nchini. Ili kufanikisha nia hiyo, na kufuatana na sheria ya nchi yetu, tumejiandikisha kama Jumuiya rasmi kwa
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na kutambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. Mategemeo yetu ni kwamba,
chombo hiki kitakuza na kuimarisha mapenzi na mashirikiano mema baina yetu na Waislamu wengine popote walipo.
Lengo letu Waislamu sote ni moja: kufuata kumjua Mola wetu na kupata radhi zake. Jumuiya yetu hii ni ya KI-DINI.
Hivyo tumetengeneza Katiba hii katika misingi ya maadili ya Qur’ani na Sunna za Bwana Mtume Muhammad (SAW).
Juhudi za kuiandikisha Jumuiya yetu hii zilianza katika mwaka 1980. Kwa bahati mbaya hatukufanikiwa wakati huo.
Lakini Mwenyezi Mungu (SW) amejaalia, kwa bidii na juhudi za ndugu zetu wa Arusha, tumeweza kuandikishwa.
Tulianza kwa kuandikisha udhamini kwa jina la MASJID ZAWIYA EL-QADIRIYA AND ISLAMIC CENTRE mnamo tarehe 7/1/1988 na
kutangazwa katika gazeti rasmi la Serikali. Jitihada ziliendelea kufanywa na ilipofika mwaka 1990, tukafanikiwa kukiandikisha
chombo hiki Wizara ya Mambo ya Ndani na kupewa Hati ya kuandikishwa Nambari S.O.7168 ya tarehe 2/11/90.
Katika Mkutano Mkuu wa kwanza uliofanyika tarehe 26/9/91 hadi 29/9/91 huko Arusha, wajumbe katika kujadili Katiba,
walikubaliana kubadili jina ili chombo hiki kitambulikane kuwa ni cha nchi nzima. Jina jipya lililokubaliwa lilikuwa
JUMUIYA ZAWIYATUL QADIRIYA TANZANIA (yaani Jumuiya ya Mazawiya ya Twariqa ya Qadiriya hapa Tanzania).
Tarehe 10/4/1992, Wizara ya Mambo ya Ndani ilitoa Hati nyingine ya uandikishaji nambari S.O.7168 kwa jina jipya.
Ofisi ya Kabidhi Wasii Mkuu wa Wadhamini nayo tarehe 9/11/1992 ilitoa Hati mpya kwa jina jipya na kutangaza
katika gazeti la Serikali la tarehe 27/11/1992 ukurasa 937, tangazo nambari 947.
Misingi na chanzo cha Jumuiya hii inatokana na Twariqa. Kwa miaka mingi sasa tangu Uislamu uingie katika nchi
yetu (Al-Hamdulillah) mafunzo ya Twariqa yamekuwa yakitolewa na Mashekhe mbalimbali na taratibu zake za Ibada
zimekuwa zikifuatwa. Lakini kutokana na hali ya ulimwengu ulivyo na nyoyo kumili katika ulimwengu tukaonelea
iko haja kuzidi kukumbushana katika Dini yetu. Hivyo, katika mazingira ya aina hii, imebidi tuzidishe bidii
katika kuzisafisha nafsi zetu kwa kushikamana na Twariqa.
Muanzilishi na muasisi wa JZQT ni shekhe Muhammad nassor
Madrasa, Maahad, Scholarship(Ufadhili wa Masomo)
Ujenzi wa Misikiti, Madrasa, Nyumba
Hijja, Zakka, Sadaka, Mayatima, Visima
© www.jzqt.org - Haki zote Zimemilikiwa. Template by HTML Codex